Malkia Elizabeth II avunja rekodi ya kuongoza Uingereza kwa miaka mingi zaidi

 
Malkia huyo alieanza utawala wake mwaka 1952, ametimiza hivi leo miaka 63 ya uwongozi wake tangu aingia madarakani akiwa na umri wa miaka 25.
Rekodi hiyo aliyoiweka leo, inakuwa rekodi mpya juu ya Bibi yake Mkubwa Malkia Alexandrina Victoria.
Waziri Mkuu David Cameron amesema kuwa ataongoza hafla hiyo maalum iliyoandaliwa kwa Heshima ya Malkia huyo itakayofanyika  katika Bunge la Juu na kisha kufuatiwa na salamu za kijeshi jirani na medani za Mto Thames.
Katika hafla hiyo muhimu kwa Malkia Elizabeth, atatumia gari alilotumia bibi yake mkubwa katika hafla yake kama hiyo karne za nyuma.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment