Majaji wa ICC watupia mbali ombi la mwanasheria wa Gbagbo

Gbagbo alikuwa Rais wa Ivory Coast kabla ya kufikishwa katika mahakama ya kimataifa. Hii inatokana na yeye kukataa kutoka madarakani baada ya kushindwa Urais dhidi ya mpizani wake, jambo ambalo lilisababisha machafuko katika nchi hiyo na watu wengi kupoteza maisha kutokana na vita katikati yao.
Gbagbo alikamatwa mwaka 2011 na kupelekwa kizimbani mwaka huo huo.
Mapema Jumanne hii jopo la Majaji watatu lilizitupilia mbali hoja zote zilizotolewa na mwanasheria wa Gbagbo kuomba  dhamana ya muda mfupi. Uamuzi huo uliotolewa awali unaoruhusu Gbagbo kuendelea kuwa kizuizini ulikuwa halali kwani iwapo ataachiwa kwa muda wowote lolote laweza kutokea kabla hukumu dhidi yake haijatolewa.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment