Makocha saba wakigeni kuonekana katika Ligi kuu msimu 2015/16



Maandalizi ya ligi kuu bara yamezidi kushika kasi baada ya timu nyingi zinazoshiriki ligi kuu msimu wa 2015/16  kusaini mikataba na makocha wa kigeni.
Usajiri huo wa makocha hao umekuwa kivutio kikubwa kwa wapenzi wa soka na hata kwa mashabiki, kwani mashabiki hao wamejazwa na shauku kubwa ya kuona nini makocha hao wataleta katika ligi kuu hii inayoanza tarehe za usoni.
Baadhi ya makocha waliosajiliwa ni kama Martin  Glerics kutoka (Uingereza)  atakaefundisha Toto Africa, Stewart Hall (Uingereza) atakaefundisha Azam, Hans Pluijm (Mholanzi) atakaefundisha Yanga, Patrick Liewg (Mfaransa) atakaefundisha Stand United, Dylan Kerr (Uingereza) atakaefundisha Simba na Mika Lonnstrom (Finland) atakaefundisha Majimaji.Mashabiki wa timu husika wanaamini uwepo wa makocha hao nchini utawapa changamoto makocha hao wazawa na hivyo kuinua soka la Tanzania.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment