VARDY KUBAKI LEICESTER


Kwa kipindi kirefu Arsenal Wenger amekuwa akiwania saini ya Vardy kutoka Leicester City, kocha huyo aliamini kwa dau la paund mil 20 ingekuwa rahisi kumnasa mchezaji huyo.

Lakini bahati mbaya, harakati zake zimeshindwa kuzaa matunda kutokana na mkali huyo kudhamilia kubaki Leicester. 

Ikumbukwe Vardy alikuwa silaha kubwa ya kocha Claudio Ranieri msimu uliopita akitia wavuni magoli 24 yaliyoiwezesha Leicester kunyakua ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza EPL.

Mchezaji huyo sasa anaitumikia timu yake ya taifa ya Uingereza katika mashindano ya UERO yanayoendelea nchini Ufaransa.

Habari hii imeandaliwa na mwandishi wetu HASHIMU CHAMBUSO
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment