LUKAKU AIZAMISHA IRELAND


Mshambuliaji huyo wa Everton Romelu Lukaku ashinda mabao mawili akiisaidia timu yake ya Ubelgiji dhidi ya jamhuri ya Ireland.

Lukaku alifunga goli la kwanza dakika ya 48 ya kipindi cha pili huku goli la pili wakipata dakika ya 61 kupitia Witsel na kwa mara nyingine tena katika dakika ya 70 ya mchezo Lukaku aliifungia timu yake ya taifa.

Kwa ushindi huu unaiweka ubelgiji nafasi ya pili kwenye kundi E wakiwa na point 3 nyuma ya Italia wanaoongoza kwa point 6.

Mechi inayofuata ya Ubelgiji ni dhidi ya Sweden inayoongozwa na Zlatan Ibrahimovic siku ya Jumatano.

Habari hii imeandaliwa na mwandishi wetu Hashim Chambuso
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment