Tumezoea kusikia neno
“unyanyasaji katika mazingira mbalimbali hasa katika maisha ya kila siku. Kila
mtu akiwa na dhana yake. Wengine wakimaanisha kutokuwa na haki fulani katika
kazi au nyumbani, vilevile wengine wakiwa na maana ya kutokupewa muda wa
kutosha katika kazi ama shughuli fulani; na wengine wakiwa na maana kadha na
kadha.
Kwa ujumla hali ya unyayasaji ni hali ya
kutokupata kwa muda haki za msingi. Wafanyakazi wa kazi za ndani, mara nyingi
huchukuliwa kama wanawake/wasichana ambao wanafanya kazi mbalimbali za ndani,
vilevile huchukuliwa kama wasaidizi wa kazi za ndani pamoja na watoto wadogo
ambao wanakuwa wanahitaji uangalizi wa karibu kutoka kwa wazazi wao mara nyingi
kina mama. Wazazi wengi wa kike wanakua na kazi nyingi kiasi cha kushindwa
kumudu kazi zingine za nyumbani. Hivyo hujikuta wakihitaji wasaidizi ambao
hulazimika kuwalipa kwa namna moja au nyingine. Mara nyingine huenda na kumlea
msichana wa kazi kwani wengi wao huwa ni wadogo kiumri ambao kwa mujibu wa
sharia taratibu. Je hapo tuite ajira haramu wakati wanasaidia kazi za nyumbani?
La hasha
Ni utaratibu ambao
tumejijengea kuwalipa ujira kidogo pamoja na kuwapa mahitaji ya msingi haina
maina ya kuwa ni mfanyakazi, kwani mfanyakazi lazima awe ameandika mkataba na
muajiriwa, pia awe na umri usipungua miaka 18 na vilevile awe amejiunga na mojawapo
ya vyama vya wafanya kazi kama CWT,
wafanyakazi serikalini au kwigeneko.
Hivyo kutokana na sababu
ya kawaida wafanyakazi hawana sifa tajwa hapo juu. Hebu tuwaite wasaidizi
wakazi za nyumbani. Mara nyingi hutafutwa ili kupunguza uzito wa kazi za
nyumbani ikiwa ni pamoja na kazi za ndani, kuangalia bustani pamoja na
uangalizi wa watoto nyumbani.
Hakuna asie kuwa na kazi
za ndani ni nyingi, zinpoteza muda. Vilevile hakuna ubishi kwamba malezi ya
mtoto yanahitaji umakini wa hali ya juu pamoja na kupoteza muda.
Hivyo hawa wafanyakazi wa
ndani wanapaswa kulipwa kiasi kikubwa cha fedha, kupewa muda wa kufanya mambo
yao ya kijamii ili wawe na tija katika kazi zao za ndani na nje.
Kinyume na matarajio
haya; hawa ndio wamekua watu wa mwisho kabisa katika kulipwa kwani wengine
wanalipwa kuanzia elfu ishirini na kuendelea kwa mwezi. Mfano mfanyakazi mmoja
anaishi Tabata mawenzi, jina kapuni ameonesha namna ambavyo anaishi na familia
yake mpya ya kazi, ambapo anafanya kazi saa kumi alfajiri, anafanya kazi bila
kupumzika, vilevile anapewa chakula ambacho kimelala siku tatu.
Binti huyu bado ni mtoto mdogo ambaye ana umri
wa miaka kumi na tatu, kiasi kwamba hata elimu ya msingi hajamaliza. Ilipaswa
awe darasa la sita ambapo hata kimakuzi bado hajamaliza makuzi kimofolojia
kiasi kwamba anahitaji chakula bora pamoja na usingizi mzuri,ili akue vizuri.
Kama amekosa vitu
hivyo,je unafikiri ataweza kufanya kazi katika ufanisi bora?Dhana ya
unyanyasaji inajitokeza wazi pale mfanya kazi anapokosa ujira wake
mzuri,ananyimwa muda wa kucheza pamoja na kushirikiana na watu wengine.Waajiri
hawa wanafuata mawazo ya mwanafilosofia wa hoja ya kisayansi;Fredrick Taylor
ambaye ana amini mfanya kazi lazima umuwekee sharia za kumbana ndio afanye
kazi,kitu ambacho hakiwezekani,binadamu sio mashine,lazima mawazo ya
mwanafilosofia mwingine wa hoja ya kiutawala,mfaransa Henry Fayol ambaye
anasema kuwa mfanyakazi lazima apewe muda wa kutosha pamoja na kufanya kazi kwa
ushirikiano.
Ukiachana na mfanyakazi
huyo,yupo mwingine ambaye anaendelea kuthibitisha unyanyasaji wa wafanyakazi wa
ndani.Huyu anatoka kimara baruti,ambapo ananyimwa muda wa kutosha pamoja na
mshahara au ujira mdogo.Tofauti na aliyepita huyu [jina kapuni] ana miaka 22
hakupewa mshahara wake kwa mdaa wa miezi miwili,hivyo hakuona umuhimu wa
kuendelea kufanya kazi bila kujaliwa.Kwa mfano hiyo dhahiri tunaona kwamba
wafanyakazi wa ndani wanafanya kazi nzuri na ngumu,Bila hata chembe ya aibu na
bado wanaangaliwa kwa jicho lisilokuwa na huruma.
Kutokana na hayo tunaona
matatizo yanayojitokeza kutokana na unyanyasaji wa wafanyakazi wa ndani. Ndani
nani je ya nchi. Tukianza na ndani ya nchi, mkoani Tanga, mfanyakazi mmoja wa
ndani aljikuta akimalizia hasira zake kwa kumuwekea gundi kali “super glue”
katika sehemu zake za siri, ambapo mtoto huyo mwenye miaka mitano, alikaa nayo
kwa muda wa wiki mbili, na kuanza usikia maumivu ya tumbo na kibofu. Hili jambo
ligundulika kupitia mtoto jinsi alivyokuwa anatembea.
Namalizia kwa kuangalia
upande wa serikali, serikali hadi sasa hivi imeshindwa kuonesha makucha yake
yake katika kukomesha vitendo hivi vya kikatili kwa wafanyakazi wa ndani.
Wizara ya ajira na utumishi wa umma haina budi kufuatilia kwa ukaribu namna
wafanyakazi wa ndani wanavyopatikana kwa kusaidiana na wizara ya jinsia na
watoto. Kwani hii ni utumilikishwaji na ni ajira kwa watoto.
Makala hii imeandaliwa na mwandishi wetu Yokibeth Msuya.

0 comments:
Post a Comment