Na
Alicia Evance.
Maendeleo
katika sekta ya sayansi na teknolojia ni moja ya harakati katika nchi za Afrika
na imeweza kuinua sekta ya mawasiliano.
Katika
moja ya matunda ya harakati hizi jamii ya watu wa Afrika hasa Tanzania imeweza
kubadili mfumo wa mawasiliano kutoka analojia kwenda digitali, ingawa ilikuwa
ni harakati ngumu kufanikisha lakini Tanzania imeweza kupiga hatua na kuwa
katika hadhi moja na nchi zingine za Afrika na hata bara la Ulaya.
Kwa
kipindi cha miaka mitano ya digitali jamii imepokea maingizo tofauti ya simu
kwa ajili ya mawasiliano, lakini toleo hili la simu aina ya ‘bakobako’ limepokelewa
kwa kiasi kikubwa na jamii hasa vijana kuliko toleo zilizotangulia.
BakoBako
yaweza kuwa sio jina sahihi lakini ni maana moja na majina tofauti kwa simu za
mkononi yaani“smartphone” na hii ni kutokana na tofauti ya upokeaji wa simu
hizi katika jamii, lakini pamoja na majina hayo tofauti jina la BakoBako
limeenea sana katika kanda zote za Tanzania.
Takwimu zilizofanywa na vituo
mbalimbali kama Pew research center tangu mwaka 2014 zinathibitisha matumizi ya
simu aina BakoBako hasa kwa vijana kuliko simu za kawaida kama nokia tochi na
mnara.
Kutokana
na utafiti huo imetambulika kuwa asilimia 70 ya watu katika jamii wanaotumia
simu za aina hii ni vijana na ni asilimia 30 ya wanajamii waliosalia wanatumia
simu za kawaida, ikiwa asilimia 20 kati ya 30 ni wanawake wenye kipato cha chini
na asilimia 10 iliyobaki ni wanaume wenye hali kama hiyo.
Uchunguzi
unaonesha kuwa, kati ya asilimia 70 ya vijana wanaotumia aina hii ya simu
huegemeza matumizi yao na kutumia muda mwingi katika kutuma ujumbe mfupi kuliko
kufanya mambo ya kimaendeleo na wengi wao kutumia simu hizo katika mitandao ya
kijamii ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka kwa maadili katika jamii
kama inavyoonyesha katika jedwali.
“BakoBako
zinamatumizi tofauti kwa watu tofauti, lakini kutuma ujumbe, kuchukua picha na video
na kuingia katika mitandao ya kijamii ndio matumizi makubwa yanayofanywa na
asilimia kubwa ya vijana wanaomiliki simu hizi”
Kwa
takwimu hizi ni dhahiri kwamba vijana hupoteza muda pamoja na pesa kwa kufanya
mambo yasiyo ya maendeleo katika simu zao na hivyo kuleta hasara kubwa katika
jamii.
“Pamoja
na takwimu hizi za matumizi ya simu, jamii na wanaharakati hawajapambanua bado
fikra zao, kwanini vijana pekee ndiyo wanaoharibika? Kwani hapo kabla kijana wa
miaka 15 hakuruhusiwa kumiliki simu lakini hii leo mtoto wa miaka 12 anayejiita
kijana anamiliki simu ambayo hata mimi sijawahi kumiliki” alisema kijana
aliyejitambulisha kwa jina moja la Khamis (35).
Pengine
maneno ya Khamisi yanaweza yasifuatiliwe lakini ni jambo gani hasa mtoto wa miaka
12 anajifunza katika simu? ni kama
mtindo sasa vijana kupiga picha za utupu na kuweka mitandaoni, kusambaza video
ambazo hazina mafunzo kwa jamii na pia kutuma ujumbe usio na maadili, kwa hili mtoto huyu wa miaka 12
anajifunza nini.
Tanzania
haina budi kujilaumu lakini jamii itazame jambo hili kwa darubini ndani ya bahari,
kumruhusu kijana au mtoto wa miaka 12 kumiliki simu aina ya Bakobako
kumfungulia akaunti na pengine hufungua mwenyewe katika mitandao yote ya
kijamii na kujiunga na
makundi tofauti bila kujua mipaka yake kwa umri huo anatakiwa kuishia wapi katika
elimu ya dunia.
Bi.Rozalia
anatazama jambo hili kwa upevu wake, akiwa ni miongoni mwa watu wanaotumia
bakobako anasema “vijana wanaamini kwamba ni wakati wa mapinduzi ya utandawazi,
wanatakiwa kujua kila kitu mzee anachojua, wanaamini kwamba kijana hafunzwi na
jamii bali simu inamfunza kila kitu”.
Maneneo
haya yaweza kuwa kweli kwani asilimia kubwa ya masomo hufundishwa; “google,
wikipedia, youtube na browser”, hili pengine pia huwapa kiburi vijana lakini,
yale wanayojifunza huko sio sahihi kwa muda wao kujifunza, kama kijana
anajifunza kila kitu katika mitandao kuna haja gani ya msemo, asiyefunzwa na
mamaye ulimwengu utamfunza?
Vijana
kama nguvu kazi ya taifa wanatakiwa kuwa mfano katika matumizi bora ya simu
zao, kijana wa miaka 13 hadi 17 anatumia BakoBako kwa ajili ya mitandao ya
kijamii inamsaidia nini? ingawa mjadala utarudi palepale lakini suluhisho ni
kuweka umri sahihi wa kijana kuanza kumiliki simu na kumiliki akaunti zake
katika mitandao, lakini ni wangapi wataunga mkono jambo hili?
Kijana
anatakiwa kufahamu matumizi sahihi ya simu kulingana na umri na wakati wake wa
kujifunza na kutambua mambo kwa undani na kwa manufaa zaidi kuliko kupoteza
pesa kununua vocha na muda mwingi kwa ajili ya picha, video na ujumbe usiokuwa
na manufaa na hivyo atumie muda huo kwa ajili ya kutafuta njia ya kuleta
maendeleo katika jamii.
0 comments:
Post a Comment