JE USOMI KWA MWANAMKE NI KUKIMBIA ASILI YAKE?




Na Alicia Evance.


Unawezaje kuuishi uanamke wa zamani wakati wewe ni msomi? ni kwanini unafanya shughuli zote za ndani na umeelimika? unawezaje kuishi maisha ya dhiki ili kumtumikia mwanaume aliyekuoa wakati wewe mwanamke ni msomi?
Niliyapanga vizuri maswali haya wakati nilipopatiwa nafasi ya kuendesha mjadala uliopangwa kuhudhuriwa na wanawake wasomi ambao baadhi yao ni wanawake wenye hadhi kubwa na heshima pia hapa nchini.
Ingawa mjadala haukufanyika kama ulivyotakiwa lakini kuna kitu nilijifunza kutoka katika maandalizi ya mjadala huu, timu nzima ya maandalizi ilinifunza jambo juu ya fadhila ya usomi kwa mwanamke na thamani yake kwa jamii.
Ni takribani miaka 41 tangu elimu ya jinsia na usawa ianzishwe nchini Tanzania lakini ni asilimia 60 tu ya wanawake waliofanikiwa mpaka hii leo ingawa bado jitihada zipo zakufanikisha maendeleo kwa mwanake nchini lakini, serikali inaangalia madhara ya elimu hiyo kwa mwanamke? Je mwanamke anatambua lengo la serikali kumpatia kipaumbele katika elimu?
Mjadala uliofanyika mwaka 2012, septemba na taasisi ya wanawake na maendeleo(WAMA), mama Salma Kikwete akiwa ni mwenyekiti wa taasisi hiyo alieleza faida ya elimu kwa mwanamke kwamba, ni kwa ajili ya kumuwezesha mwanamke kupambanua matatizo yaliyopo katika jamii ikiwa ni pamoja na ujinga, magonjwa na umaskini na siyo kupindua jamii yake.
Hili ni jambo la kipekee sana na yapaswa mtu kufurahi na kushukuru unapozaliwa mwanamke, si kwamba wanaume hawana thamani kwa jamii la hasha, mwanamke amekuwa akitazamwa kama mboni angavu kwa karne zaidi ya kumi.
Bi. Edna Henry ni mjasiriamali na ni mhitimu wa shahada ya uuguzi lakini, aliamua kuachana na kasumba ya usomi kama ilivyo kwa wanawake wengi na kuitazama jamii yake na kutambua inahitaji kitu gani.
“Mateke ni fadhila  ya punda” alisema Bi.Edna na kuongeza, “mimi kama mtanzania na pia mwanamke msomi sina budi kudumisha utamaduni wangu, elimu yangu isinifanye kudharau tamaduni yangu na kushusha thamani yangu kama mwanamke”.
Hakika kila mwanamke anapaswa kujifunza katia hili, ebu tujiulize maswali haya, hii wapi thamani ya mwanamke msomi? kama yeye mwenyewe ataishusha thamani ya jamii na kudharau utamaduni wake, nani atamuinua na kusema ameelimika? kuna jambo ambalo wanawake hatujaelewa bado.
Thamani ya mwanamke ni kubwa kulinganisha na kitu chochote ndani ya jamii, fadhila yake ya usomi kuwa mateke kwa jamii iliyomuinua sio jambo la kupendeza hata machoni kwa wanawake wengine waliosoma na hata ambao hawakupata nafasi hiyo ya kusoma.
Kasumba ya usomi wa mwanake kutotaka kufanya kazi zinazomuhusu hususani zile za ndani, suala la kuhitaji hamsini kwa hamsini na kusahau majukumu yake muhimu ni jambo lisilokuwa na faida, inatupasa kukumbuka na kuheshimu jiko la kale pale unapopata jipya.
“Elimu ni jambo zuri na la kimabadiliko kwa mwanamke kwani ni kwa kupitia elimu hiyo mwanamke anaweza kupambanua mambo yasiyosawa katika jamii na kujitambua lakini, hulka ya mwanamke isibadilike kutokana tu na usomi wake”, alisema mwanmke mjasiriamali aliyejitambulisha kwa jina la Bea Mwombeki.
Kutoa mjadala huu sio kwamba naunga mkono mfumo dume la hasha naitaji wanawake kutambua thamani yao katika jamii, fadhila ya usomi isiwe mateke ya kuleta hasara na kupindua jamii na tamaduni kwani, itakuwa sawa na kurudi katika utawala wa kikoloni na tumeshasherehekea miaka 54 ya uhuru wa Tanzania.
Mkuu wa maktaba ya hospitali ya KCMC, Moshi Kilimanjaro, ni moja kati ya mifano bora kwa jamii katika hili, ni mama wa mtoto mmoja na anaishi pamoja na mume wake Bw. Musa Rajabu, ingawa Bi. Tina Henry ni msomi na ni mfanyakazi ila hajasahau majukumu yake kama mama.
Bi.Tina anatambua faida za elimu kwa mwanamke na pia anathamini nafasi yake kwa jamii na familiya yake, anweka bayana kuwa, mpangilio wa kazi na muda ni muhimu kwa mwanamke, “inawezekana kabisa kuishi maisha ya dhiki na mume wa ndoa na kumtumikia kama mwanamke kwa kupangilia muda wa familiya na muda wa kazi, malengo na ratiba ndiyo vitu vinavyomkamilisha mwanamke msomi” alisema Bi. Tina.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 80 ya wanawake wasomi wamesahau wajibu wao katika jamii na hivyo kujikuta wakidharirika, kutaka hamsini kwa hamsini sio jambo baya ila, lengo ni nini? kumuinua mwanamke au kuondoa upekee wake?.
Jambo zuri la kuelewa hapa ni kwamba, mwanamke msomi ni mwanga kwa jamii na familiya hivyo mwanga huu unatakiwa kutopotosha malengo na ndoto za wale wanaoufuata mwanga huo bali umulike na kuweka wazi matunda yaliyobora kwa kujenga na kuweka  imara malengo na ndoto za jamii na familiya.
Makala hii imeandaliwa na Alicia Evance mwanafunzi wa Shule kuu ya Habari na Mawasiliano kwa umma
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment