Kiswahili lugha adhimu, kitumike vyuo vikuu.


Ndugu msomaji karibu ujumuike name katika makala yangu inayojadili nafasi ya lugha ya Kiswahili na umuhimu wake katika matumizi hasa vyuo vikuu.

Kwa kuanza ni shauku yangu kukujuza kwamba vyuo vikuu ni miongoni mwa taasisi za juu za elimu ambapo watu hujiunga ili kusomea taaluma Fulani kwa kina Zaidi. Mara nyingi taaluma hizo hutolewa katika kiwango cha shahada, aidha stashahada nazo hutolewa. Mfano wa vyuo vikuu  ni kama chuo kikuu Dodoma(UDOM),SAUT na UDSM.

Lugha ya Kiswahili ni miongoni mwa lugha za kibantu, lugha yenye historia ndefu yenye manufaa makubwa kwa Taifa la Tanzania. Chimbuko la Kiswahili huelezwa kuwa ni upwa  wa Afrika Mashiriki na baadae kusambaa sehemu nyingi Duniani.

Tunapozungumzia uhuru wa Tanganyika, Tanzania ya sasa itakuwa ni dhambi kubwa tusipokumbuka Kiswahili kwani kilikuwa kiungo muhimu baina ya jamii za Tanganyika katika kupigania uhuru.

Itakumbukwa kwamba baada ya mkutano wa Berlin, bara la Afrika liliangukia mikononi mwa wa koloni, na wakoloni waliotawala Tanganyika walilazimika kujifunza Kiswahili ili kuweza kurahisisha shughuli zao, biashara za waarabu ndiyo zilifungua uwanja mkubwa wa Kiswahili kwani kila kituo walichopita waarabu kilikuwa kikubwa cha Kiswahili.

Matumizi ya lugha ya Kiswahili hasa katika taasisi za elimu ya juu (yaani vyuo vikuu) yamekuwa yakiridhishwa na yanakumbwa na changamoto lukuki ambazo zinahatarisha maendeleo ya Kiswahili.

Sioni ubaya wa kuruhusu matumizi ya Lugha ya kiswahili kama lugha ya kufundishia katika taasisi ya elimu ya juu hususani vyuo vikuu, lugha ni sehemu ya utamaduni hivyo kama hatutumi lugha ya kiswahili katika mazingira ya wasomi tupo tayari kuu kana utamaduni wetu.

Kuna Imani miongoni mwa watu kuwa lugha ya kiingereza ndio lugha inayofaa kutumika kufundishia vyuo vikuu, kuwapatia watu elimu na maarifa ya kufanya kazi na ndiyo lugha ya biashara au ajira, kwangu mimi naona mtazamo huu kama potofu, uliotawaliwa na ufinyu wa mawazo kwa yupo mwanasaikolojia mmoja alisema “mtu akifundishwa kwa lugha yake ya asili kisukuma, ataelewa Zaidi.” Na mahanisha lugha yetu ya kiswahili inajitosheleza kuwajuza watu elimu kwa manufaa ya taifa.

Ingawa sera ya kufundishia vyuo vikuu ni lugha ya kiingereza bado ni changamoto kubwa kwa walimu, sisemi kuwa hawajui kiingereza la hasha bali ninachotaka kusema hapa ni kwamba baadhi yao ambao ni asilimia kubwa hupenda kuchanganya lugha (code mixing) katika mihadhara yao wanaotoa. Sio kosa lao kwani kazi ya mwalimu ni kumfanya mwanafunzi aelewa kwa namna yiseyote na matumizi ya lugha zote mbili yaani kiswahili na kiingereza ni moja jitihada hizo. Ni dhahiri shahiri kuwa lugha ya kiswahili ni lugha ya Taifa, kutokana historia ya lugha hii kuwaleta watu pamoja ndiko kunakonifanya nijiuliza kwanini kiswahili kitumike kwa kuibuiba wakati ni lugha rasmi ya Tanzania?

Aidha wataluma wa lugha hudai kwamba mtoto hujifunza na kuielewa lugha kwa ufasaha zaidi, kuliko mtu mzima. Ni wazi kwamba mfumo wa Tanzania wa elimu kuanzia elimu ya vidudu au chekechea hadi darasa la saba ambapo kiingereza ni kama somo tuu, huku lugha ya kiswahili ikichukua nafasi kubwa. Katika kipindi hicho mtoto ndio ana uwezo mkubwa wa kuifahamu lugha kwa umakini, cha ajabu ni kuifanya kiyume pindi aingiapo kidato cha kwanza hadi chuo kikuu, ambapo kiswahili hufundishwa kama somo na masomo mengine kutumia kiingereza.

Maendeleo ya nchi yeyote ile huletwa na wataalamu wake waliofundishwa kwa lugha za nchi zao na kuelewa na kubobea. Mfano ni nchi kama China, Korea na Urusi ambazo zinamaendeleo ya juu kutokanana na kuzingatiia matumizi ya lugha zao. Hivyo kama nasi tukiipa kipaumbele lugha yetu ya Taifa basi na sisi kuna uwezekano mkubwa wa kupata kuendelea kichumi kama nchi taja katika aya hii.

Wahenga walisema safari ni hatua na waswahili husema tunajifunza kutokana na makosa. Sioni kama vibaya kwa Tanzania kuiga baadhi ya sera nzuri zitakazo ifanya lugha ya kiswahili, lugha adhimu kuzidi kuwa na mashiko katika nchi yetu. “sera ya  matokeo makubwa sana”  ilianza nchini Malaysia na imeleta mafanikio makubwa na sasa naona ni wakati  muafaka kwa nchi ya Tanzania kukopa sera ya lugha kutoka nchi za magharibi ilikuendeleza na kukuza lugha ya kiswahili. Kwani kwa kukopa huko kutachangia katika ukuzaji wa uchumi na kupunguza matabaka ndani ya nchi.

Kwa kumalizia Makala haya, huenda wengine watakosoa matumizi ya lugha ya kiswahili chuo kikuu.Kikubwa nachotaka kusema ni kuwa Kiswahili inajitosheleza na inahadhi kulinganisha na soko la kimataifa. Pia lugha yoyote inayokuwa lazima ikope msamiati mingine toka lugha zingine hivyo waandishi wa vitabu vya somo lolote lile kwa manufaa ya Taifa letu na ili yote haya kufunikiwa lazima sera ya elimu itazamwe upya na waandichi kuondoa kusumbaa na kuona lugha ya kiswahili ni duni na kuzikweza lugha za mataifa mengine.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment